TASSO kutoshugulika na maandalizi na Usimamizi wa Nane Nane.

In Kitaifa
Zikiwa zimebaki siku chache kabla ya kuanza  sherehe za wakulima Nane Nane  Kanda ya Kaskazini, Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo ametoa tamko la TASSO kutoshugulika na maandalizi na Usimamizi wa sherehe hizo kama miaka mingine iliyopita kutokana na Usimamizi Usioridhisha  kwa Wakulima
Akizungumza  na Wakuu wa Wilaya, na Wakurugenzi wa Kanda ya Kaskazini katika kikao cha pili cha Maandalizi ya Sikukuu ya Wakulima,Gambo  amesema sababu ya serikali kuwaondoa TASSO ni kutokana na usimamizi hafifu ambao umekuwa ukifanywa na TASSO kwa nchi nzima.
Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Manyara John Bendera amesema kanda ya kaskazini imepokea agizo la serikali bila vipingamizi hivyo watahakikisha shughuli hizo zinafanyika  kwa ufanisi mkubwa.
Nae mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Mh. Anna Mgwira amesema ili kuweza kukamilisha zoezi hilo ,panatakiwa kuwa na ulinzi na usalama wa kutosha ,ambapo amewataka wakulima wajiandae ikiwa ni pamoja na kubadilisha bidhaa zao kutoka malighafi kuingia viwandani.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

NACTIVET YASIMAMISHA MAFUNZO CHUO CHA MBEYA TRAINING..DC MALISA AAGIZA KUFANYIWA UHAKIKI VYUO VYOTE WILAYA YA MBEYA

Wazazi Wanafunzi na wahitimu wa chuo cha Mbeya training wameiomba serikali iwasaidie kurudishiwa stahiki zao mara baada ya kubainika

Read More...

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMANNE NOVEMBA 7, 2023

Manchester United na Newcastle United zote zinamfuatilia mshambuliaji wa Lyon Mfaransa Rayan Cherki, 20, ambaye mkataba wake unamalizika Juni

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu