TASSO kutoshugulika na maandalizi na Usimamizi wa Nane Nane.

In Kitaifa
Zikiwa zimebaki siku chache kabla ya kuanza  sherehe za wakulima Nane Nane  Kanda ya Kaskazini, Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo ametoa tamko la TASSO kutoshugulika na maandalizi na Usimamizi wa sherehe hizo kama miaka mingine iliyopita kutokana na Usimamizi Usioridhisha  kwa Wakulima
Akizungumza  na Wakuu wa Wilaya, na Wakurugenzi wa Kanda ya Kaskazini katika kikao cha pili cha Maandalizi ya Sikukuu ya Wakulima,Gambo  amesema sababu ya serikali kuwaondoa TASSO ni kutokana na usimamizi hafifu ambao umekuwa ukifanywa na TASSO kwa nchi nzima.
Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Manyara John Bendera amesema kanda ya kaskazini imepokea agizo la serikali bila vipingamizi hivyo watahakikisha shughuli hizo zinafanyika  kwa ufanisi mkubwa.
Nae mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Mh. Anna Mgwira amesema ili kuweza kukamilisha zoezi hilo ,panatakiwa kuwa na ulinzi na usalama wa kutosha ,ambapo amewataka wakulima wajiandae ikiwa ni pamoja na kubadilisha bidhaa zao kutoka malighafi kuingia viwandani.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu