Tatizo la nguvu za kiume zatinga bunge.

In Afya, Kitaifa, Siasa

 

Sakata la upungufu wa nguvu za kiume ambalo limekuwa changamoto kubwa kwa baadhi ya wanaume nchini, limeibua sintofahamu bungeni leo.

 

Hali hiyo imeibuka baada ya mbunge wa Konde Khatibu Saidi Haji kupitia CUF, kutaka kujua serikali imejipanga vipi katika kukabiliana na tatizo hilo.

Akijibu swali hilo Naibu waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Daktari Hamisi Kigwangala, amekiri kuwepo kwa tatizo hilo na kusema kuwa, serikali haina jibu la moja kwa moja kuweza kuwapa wananchi, kwani tendo la ndoa hufanyika faragha baina ya wanandoa.

Dkt Kigwangala ameeleza pamoja na usiri uliopo kuhusu tatizo hilo, lakini kuna vitu wanaweza kufanya ili kukabiliana nalo, ambapo huwenda likasaidia kuokoa ndoa na kuweza kuwapatia wanandoa watoto.

Baada ya Dr Kigwangala kutoa maelezo hayo,kwa upande wake  waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu, amesema serikali imepiga marufuku waganga wa tiba za asili nchini na wadau mbalimbali, ambao wanauza dawa zinazodaiwa kuongeza nguvu za kiume kinyume na sheria.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu