Tatizo la nguvu za kiume zatinga bunge.

In Afya, Kitaifa, Siasa

 

Sakata la upungufu wa nguvu za kiume ambalo limekuwa changamoto kubwa kwa baadhi ya wanaume nchini, limeibua sintofahamu bungeni leo.

 

Hali hiyo imeibuka baada ya mbunge wa Konde Khatibu Saidi Haji kupitia CUF, kutaka kujua serikali imejipanga vipi katika kukabiliana na tatizo hilo.

Akijibu swali hilo Naibu waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Daktari Hamisi Kigwangala, amekiri kuwepo kwa tatizo hilo na kusema kuwa, serikali haina jibu la moja kwa moja kuweza kuwapa wananchi, kwani tendo la ndoa hufanyika faragha baina ya wanandoa.

Dkt Kigwangala ameeleza pamoja na usiri uliopo kuhusu tatizo hilo, lakini kuna vitu wanaweza kufanya ili kukabiliana nalo, ambapo huwenda likasaidia kuokoa ndoa na kuweza kuwapatia wanandoa watoto.

Baada ya Dr Kigwangala kutoa maelezo hayo,kwa upande wake  waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu, amesema serikali imepiga marufuku waganga wa tiba za asili nchini na wadau mbalimbali, ambao wanauza dawa zinazodaiwa kuongeza nguvu za kiume kinyume na sheria.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu