TEMBO WAUA TENA KIGONIGONI

In Kitaifa

Aliyekuwa mwananchi wa Kijiji cha Kigonigoni Wilayani Mwanga Mkoani Kilimanjaro, Yonael Kaindu Maarufu kama Mzembi, ameshambuliwa na Kuuawa na Tembo asubuhi ya leo August 3 2022.

Yonael na Wenzake wa (3) ambao ni Dhihiri Rajabu, Jonson Mtwatui na Peter Jacob walikuwa wakielekea Ziwa Jipe kwa ajili ya Shughuli zao za kila siku za Uvuvi ambapo walivamiwa na Tembo hao na Tembo Kumuua huku wenzake wakibahati kuokoka kwa Kukimbia na Kupanda kwenye Miti.

Hata hivyo Matukio ya watu kuuwawa yamekithiri katika Vijiji hivyo Jirani vya Kigonigoni, Kwakoa, Ngulu, Butu, Ruru na Toloha ambapo Mpaka sasa zaidi ya Watu 10 wamepoteza maisha kwa Matukio ya Tembo hao ambao Wamezagaa kila Mahali huku Wananchi wakilalamikia Serikali kutochukua Hatua.

Jeshi la Polisi pamoja na Tanapa wamefika eneo hilo na Kuuchukua mwili wa Marehemu kwa ajili ya Uchunguzi zaidi ambapo baada ya kufika kumetokea Vurugu kati ya Wananchi na Polisi kwa kile wananchi walichosema Wamechoka Matukio haya Kujirudia ambapo baadae Polisi waliwatuliza wananchi na kusema Watachukua hatua.

Ukiachana na Matukio ya Kuuwawa Watu, Tembo hao wamewatia Wananchi Umaskini katika Vijiji hivyo ambapo wamekuwa wakiharibu Mazao kila Msimu kitu Kinachofanya Wananchi hawana Chakula.

Tunaendelea Kumtafuta RPC wa Kilimanjaro, Mkuu wa Wilaya ya Mwanga na Mbunge wa Mwanga

Imeandikwa na Hamis A. Hamis

Radio5Updates @radio5tz

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu