Kocha wa Tottenham Jose Mourinho ana matumaini ya kuipiku
Manchester United kumsajili kiungo wa RB Leipzig Emil
Forsberg, 28. (Express)
Real Madrid wanaamini wataweza kumsajili mshambuliaji wa
Liverpool na timu ya taifa ya Misri, Mohamed Salah, 27 kwa
kitita cha pauni milioni 126 baada ya kuachana na mshambuliaji
Gareth Bale, 30 (El Desmarque, via Express)
Manchester United wanajiandaa kumuuza kiungo Jesse Lingard,
27, na Andreas Pereira, 24, kwa ajili ya kugharamia uhamisho
wa kiungo Jack Grealish,24. (Express)
Arsenal imejaribu kuanzisha tena mazungumzo na Pierre-
Emerick Aubameyang, mkataba wake wa sasa wa mshahara wa
pauni 2000,000 unatarajiwa kwisha mwishoni mwa msimu
ujao.(Times, subscription required)
Mabingwa wa Ujerumani Bayern Munich wamekuwa katika
mawasiliano na wawakilishi wa mshambuliaji wa Liverpool
Roberto Firmino,28. (Echo)
Katika hatua nyingine, Liverpool wako kwenye mazungumzo na
RB Leipzig na mshambuliaji wa Ujerumani Timo Werner, 23.
(Express)