(TLS) kumburuza Mahakamani Mkuu wa Mkoa wa Dar-es-Salaam, PAUL MAKONDA.

In Kitaifa

BARAZA la Uongozi la Chama cha wanasheria nchini Tanganyika law Society (TLS) ,linatarajia kumwandikia barua Mkurugenzi wa mashitaka nchini DPP kumshinikiza atoe ridhaa ili wampeleke Mahakamani Mkuu wa Mkoa wa Dar-es-Salaam,PAUL MAKONDA kwa tuhuma za makosa mbalimbali  ya jinai ikiwemo kutumia vyeti feki,ujambazi wa kutumia silaha na matumizi mabaya ya madaraka.

Pia Baraza hilo limesema kuwa endapo Mkurugenzi wa mashitaka nchini DPP atakataa kutoa ridhaa yake,TLS itamfungulia mashitaka ya rejea ya kimahakama katika mahakama kuu ya Tanzania ili alazimishwe kutoa ridhaa hiyo.

Kauli hiyo imetolewa leo Mjini Dodoma na Mwenyekiti wa Baraza hilo ambae pia ni Rais wa Chama cha wanasheria nchini TLS,Mh.TUNDU LISSU, wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari.

Pia amebainisha kuwa  baraza la uongozi la chama hicho limefikia maamuzi hayo baada ya kikao chake cha siku mbili na kuazimia kuchukua hatua hizo kwa lengo la kulinda utawala wa Sheria na uwajibikaji katika nchi.

Pia Baraza hilo limebainisha kuwa PAUL MAKONDA hajafanya kosa hilo tu bali kwa kitendo chake cha kuvamia ,kituo cha kurushia matangazo cha Clouds Media Group kipindi cha miezi miwili iliyopita  na kwamba amefanya makosa mengine mengi yapatayo 10 ambapo hapa anabainisha baadhi ya makosa hayo

Katika hatua nyingine pia baraza hilo limeazimia kuchukua hatua  kwakushirikiana na wadau wengine za kuhoji masuala mbalimbali ambayo yameathiri ustawi  wa jamii ya Tanzania hususan masuala ya mafao na haki za wafanyakazi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu