(TLS) kumburuza Mahakamani Mkuu wa Mkoa wa Dar-es-Salaam, PAUL MAKONDA.

BARAZA la Uongozi la Chama cha wanasheria nchini Tanganyika law Society (TLS) ,linatarajia kumwandikia barua Mkurugenzi wa mashitaka nchini DPP kumshinikiza atoe ridhaa ili wampeleke Mahakamani Mkuu wa Mkoa wa Dar-es-Salaam,PAUL MAKONDA kwa tuhuma za makosa mbalimbali  ya jinai ikiwemo kutumia vyeti feki,ujambazi wa kutumia silaha na matumizi mabaya ya madaraka.

Pia Baraza hilo limesema kuwa endapo Mkurugenzi wa mashitaka nchini DPP atakataa kutoa ridhaa yake,TLS itamfungulia mashitaka ya rejea ya kimahakama katika mahakama kuu ya Tanzania ili alazimishwe kutoa ridhaa hiyo.

Kauli hiyo imetolewa leo Mjini Dodoma na Mwenyekiti wa Baraza hilo ambae pia ni Rais wa Chama cha wanasheria nchini TLS,Mh.TUNDU LISSU, wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari.

Pia amebainisha kuwa  baraza la uongozi la chama hicho limefikia maamuzi hayo baada ya kikao chake cha siku mbili na kuazimia kuchukua hatua hizo kwa lengo la kulinda utawala wa Sheria na uwajibikaji katika nchi.

Pia Baraza hilo limebainisha kuwa PAUL MAKONDA hajafanya kosa hilo tu bali kwa kitendo chake cha kuvamia ,kituo cha kurushia matangazo cha Clouds Media Group kipindi cha miezi miwili iliyopita  na kwamba amefanya makosa mengine mengi yapatayo 10 ambapo hapa anabainisha baadhi ya makosa hayo

Katika hatua nyingine pia baraza hilo limeazimia kuchukua hatua  kwakushirikiana na wadau wengine za kuhoji masuala mbalimbali ambayo yameathiri ustawi  wa jamii ya Tanzania hususan masuala ya mafao na haki za wafanyakazi.

Exit mobile version