TRA Wawahurumia Serengeti Boys na Kuliachia basi la TFF Lenye Deni kubwa

In Michezo

Mamlaka ya mapato nchini, TRA imeliachia basi la shirikisho la soka nchini, TFF lililokuwa limekamatwa na wakala wake wa udalali, Yono kutokana na limbikizo la madeni. Kampuni ya Yono ililishikilia kwa muda basi hilo jana.

Taarifa ya TFF kupitia mitandao ya kijamii imesema: Nathibitisha kuwa Kampuni ya Udalali ya Yono ambayo ni Wakala wa TRA imetangaza kuliachia gari mara moja basi linalotumiwa na wachezaji wa Serengeti Boys na wameomba nilifuate hata sasa, usiku huu. Wamefuata amri ya TRA. Tutalifuata asubuhi, ili liendelee na shughuli mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwapeleka vijana wetu Airport kuwahi ndege kwani vijana wetu wanatarajia kuondoka jioni.

Naye Rais wa TFF, Jamal Malinzi ametweet: Basi la TFF limeachiwa usiku huu.Suala hili la kodi tukijaliwa tutalimaliza vizuri tu kwa majadiliano.Usikimbilie kuhukumu.”

Awali wao wenye TRA waliandika: TRA inasikitishwa na kitendo cha mmoja wa mawakala wa kudai madeni kwa kukamata gari ya Serengeti Boys bila kujali wala kuzingatia utaratibu. Imethibitisha agizo la kuachiwa kwa gari hiyo limetekelezwa, wakati taratibu zingine za kiutendaji zikiwa zinaendelea kwa wahusika.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu