TRA Wawahurumia Serengeti Boys na Kuliachia basi la TFF Lenye Deni kubwa

In Michezo

Mamlaka ya mapato nchini, TRA imeliachia basi la shirikisho la soka nchini, TFF lililokuwa limekamatwa na wakala wake wa udalali, Yono kutokana na limbikizo la madeni. Kampuni ya Yono ililishikilia kwa muda basi hilo jana.

Taarifa ya TFF kupitia mitandao ya kijamii imesema: Nathibitisha kuwa Kampuni ya Udalali ya Yono ambayo ni Wakala wa TRA imetangaza kuliachia gari mara moja basi linalotumiwa na wachezaji wa Serengeti Boys na wameomba nilifuate hata sasa, usiku huu. Wamefuata amri ya TRA. Tutalifuata asubuhi, ili liendelee na shughuli mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwapeleka vijana wetu Airport kuwahi ndege kwani vijana wetu wanatarajia kuondoka jioni.

Naye Rais wa TFF, Jamal Malinzi ametweet: Basi la TFF limeachiwa usiku huu.Suala hili la kodi tukijaliwa tutalimaliza vizuri tu kwa majadiliano.Usikimbilie kuhukumu.”

Awali wao wenye TRA waliandika: TRA inasikitishwa na kitendo cha mmoja wa mawakala wa kudai madeni kwa kukamata gari ya Serengeti Boys bila kujali wala kuzingatia utaratibu. Imethibitisha agizo la kuachiwa kwa gari hiyo limetekelezwa, wakati taratibu zingine za kiutendaji zikiwa zinaendelea kwa wahusika.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

NACTIVET YASIMAMISHA MAFUNZO CHUO CHA MBEYA TRAINING..DC MALISA AAGIZA KUFANYIWA UHAKIKI VYUO VYOTE WILAYA YA MBEYA

Wazazi Wanafunzi na wahitimu wa chuo cha Mbeya training wameiomba serikali iwasaidie kurudishiwa stahiki zao mara baada ya kubainika

Read More...

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMANNE NOVEMBA 7, 2023

Manchester United na Newcastle United zote zinamfuatilia mshambuliaji wa Lyon Mfaransa Rayan Cherki, 20, ambaye mkataba wake unamalizika Juni

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu