(TRA) yatangaza makusanyo ya kodi.

In Kitaifa

MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imetangaza makusanyo ya kodi kwa mwaka wa fedha 2016/17 kuwa yalikuwa Sh trilioni 14.4.

Makusanyo hayo yana ongezeko la asilimia 7.67 ya makusanyo yaliyofanywa na TRA katika mwaka wa fedha wa 2015/16 ambayo yalikuwa Sh trilioni 13.3.

Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Walipa Kodi, Richard Kayombo amesema kwa Juni ilikusanya kiasi cha Sh trilioni 1.37.

Kayombo pia amesema mamlaka imeendelea kukusanya kodi mbalimbali ikiwemo kodi ya majengo na mwitikio wake umekuwa ni wa kiwango cha kuridhisha.

Amesema aliwashukuru wananchi wanaojitokeza katika ofisi mbalimbali za mamlaka nchi nzima ili kulipia kodi hiyo ya majengo ambayo mwisho wake wa kulipa ni Julai 15, mwaka huu.

Ameongeza kuwa TRA inatoa mwito kwa wafanyabiashara wote kutoa risiti za kielektroniki (EFDs) pindi wanapouza bidhaa au huduma na wananchi wote, kuhakikisha wanadai risiti pindi wanaponunua bidhaa au huduma

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu