Trump aendelea kuikosoa China.

In Kimataifa

Rais wa Marekani Donald Trump kwa mara nyingine ameishambulia China kwa jinsi ilivyoshughulikia mlipuko wa virusi vya a corona huku akisema janga hilo limekuwa na madhara makubwa kwa Marekani. Trump amewaambia waandishi habari mjini Washington kuwa ugonjwa wa COVID-19 usingesababisha athari kubwa iwapo Beijing ingefanikiwa kuudhibiti kikamilifu ulipozuka mwishoni mwa mwaka uliopita. Kiongozi huyo amesema Marekani imeathiriwa kwa kiwango kikubwa na janga la corona kuliko mashambulizi ya mabomu dhidi ya kambi ya kijeshi ya Pearl Harbor ya mwaka 1941 au tukio la kigaidi la Septemba 11. Hadi sasa zaidi ya watu 73,000 wamekufa nchini Marekani kutokana na ugonjwa wa COVID-19 na mkuu wa zamani wa taasisi ya kuzuia magonjwa nchini humo amebashiri idadi ya vifo inaweza kufikia 100,000 mwishoni mwa mwezi Mei.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu