Trump apewa onyo

In Kimataifa

Rais mteule wa Marekani, Joe Biden ameonya kuwa hatua ya Rais Donald Trump kukataa kukubali kushindwa na kuratibu mchakato wa kipindi cha mpito cha kukabidhi madaraka, inaweza kusababisha watu zaidi kufa kwa ugonjwa wa COVID-19. Akizungumza na waandishi habari kwenye jimbo la Delaware, Biden amesema watu wengi huenda wakafa iwapo hakutakuwa na ushirikiano. Serikali ya Trump bado haijamkubali rasmi Biden kama rais mteule, hatua inayomaanisha kuwa Biden na timu yake hawawezi kupata taarifa za kijasusi kuhusu masuala ya usalama wa taifa, vile vile kuwa na mpango wa kusambaza chanjo zinazowezekana za COVID-19. Biden amesema wanapopambana na COVID, wanapaswa kuhakikisha kwamba wafanyabiasha na wafanyakazi wana rasilimali na mwongozo wa kitaifa. Biden na Makamu wa Rais mteule, Kamala Harris pia walifanya mikutano kwa njia ya video na vyama vya wafanyakazi na wakuu wa kampuni mbalimbali.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu