Trump apuuza wito wa kansela wa Ujerumani.

In Kimataifa

Rais wa Marekani Donald Trump amepuuziia wito wa kansela wa Ujerumani Angela Merkel wakusitisha vita vya maneno kati ya Marekani na Korea Kaskazini.

Merkel amekosoa mvutano unaoendelea kati ya nchi hizo mbili, akisema kwamba kuendeleza vita vya maneno kati yao si njia sahihi.

Trump amesema kwamba Marekani imejitayarisha na ipo tayari kuchukua hatua za kijeshi iwapo Korea Kaskazini itafanya mashambulizi, amewaambia waandishi habari kwamba kazi ya Merkel ni kuisemea Ujerumani.

Wizara ya mambo ya nje ya China imesema nchi yake ambayo ni mshirika mkuu wa kibiashara kwa Korea Kaskazini, inatarajia pande zote mbili zitachukue jitihada zaidi katika kupunguza mgogoro unaoendelea kwa sasa na kujenga uaminifu wa pamoja, kuliko kuonyeshana nguvu.

Trump atakutana na rais wa China Xi Jinping hapo Ijumaa na watajadili vikwazo vya kisiasa vya ziada dhidi ya taifa hilo ambalo limejitenga na dunia.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

ZOEZI LA UOKOAJI HANANG, MAWAZIRI WAFIKA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista J. Mhagama, Waziri wa Ujenzi Innocent

Read More...

RC MBEYA AFANYA UZINDUZI ZOEZI LA UGAWAJI VITAMBULISHO VYA (NIDA)

Mkuu wa mkoa wa mbeya Mhe. Comrede Juma Zuberi Homera amefanya uzinduzi wa wa zoezi la ugawaji wa vitambulisho

Read More...

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu