Trump azidisha makali ya mvutano kuhusu mradi wa nyuklia.

In Kimataifa

Rais Donald Trump wa Marekani anazidisha makali ya mvutano kuhusu mradi wa nyuklia wa Korea Kaskazini, akisema huenda onyo lake la awali dhidi ya serikali ya mjini Pyongyang “halikuwa kali vya kutosha”.

Rais Trump ameyatoa matamshi hayo akiwa nyumbani kwake, Bedminster, katika jimbo la New-Jersey.

Trump amesema Korea Kaskazini inabidi iingiwe na taharuki kubwa hata kama inafikiria uwezakano wa kuihujumu Marekani au washirika wake, akitetea vitisho alivyotoa Jumanne iliyopita dhidi ya serikali ya Kim Jong-Un.

Hata hivyo rais Trump aliyeionya Pyongyang kuwa itakabiliwa na “moto na ghadhabu kubwa pamoja na nguvu ambazo ulimwengu haujawahi kushuhudia”. Ameitolea wito kwa mara nyengine China izidi kuishinikiza Korea Kaskazini, ingawa pia alisema Marekani iko tayari kwa mazungumzo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Serikali kuunga mkono juhudi za Taasisi mbali mbali.

Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Mwinyi, amesema serikaliitaendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Taasisi yaZanzibar Maisha Bora Foundation,pamoja na

Read More...

DKT. KIRUSWA AZINDUA MFUMO WA USHIRIKISHWAJI WA WATANZANIA KATIKA SEKTA YA MADINI

Watanzania waendelea kunufaika Sekta ya Madini, ajira 15,341 zamwagwa, manunuzi ya ndani ya nchi yafikia Dola za Marekani bilioni

Read More...

MAFURIKO YAUWA 190 MALAWI

Takriban watu 190 sasa wamethibitishwa kufariki nchini Malawi baada ya Dhoruba ya Mafuriko ya Tropiki Freddy kulikumba eneo

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu