TUCTA yaiomba Serikali kuangalia kwa jicho lingine wafanyakazi zaidi ya elfu 9 waliobainika kugushi vyeti.

In Kitaifa
Shirikisho la vyama huru vya wafanyakazi Tanzania TUCTA-Mkoa wa Dar es salaam, limeiomba serikali kuangalia kwa jicho lingine wafanyakazi zaidi ya elfu 9 waliobainika kugushi vyeti ,badala ya kuwafukuza kazi kutokana na kuchangia nguvu zao katika kuleta maendeleo katika kipindi ambacho walikuwa kazini.
Ombi limetolewa na mwenyekiti TUCTA mkoa wa Dar es salaam George Faustine, wakati wa maadhimisho ya siku ya wafanyakazi Duniani mkoani humo ambapo amesema kimsingi TUCTA, haiungi mkono suala la kugushi vyeti bali limeangalia utu na heshima ya mtu lakini pia shirikisho lina wajibu wa kumtetea mwanachama wake ,ili kuweka usawa baina yake na mwajiri.
Kwa upande wake mbunge wa urambo ambaye pia aliwahi kuwa rais wa kwanza TUCTA Magreth Sitta ambaye ni mgeni rasmi katika sherehe hizo ameiambia TUCTA kuwa ijenge utamaduni wa kuendesha wenyewe shughuli za maadhimisho hayo badala ya kutegemea viongozi kutoka serikalini kwani siku hiyo inatoa fursa kwao kujadili chanagamoto zinawakabili wafanyakazi

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

ZOEZI LA UOKOAJI HANANG, MAWAZIRI WAFIKA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista J. Mhagama, Waziri wa Ujenzi Innocent

Read More...

RC MBEYA AFANYA UZINDUZI ZOEZI LA UGAWAJI VITAMBULISHO VYA (NIDA)

Mkuu wa mkoa wa mbeya Mhe. Comrede Juma Zuberi Homera amefanya uzinduzi wa wa zoezi la ugawaji wa vitambulisho

Read More...

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu