TUCTA yamtaka Rais Magufuli kutupia jicho sekta binafsi.

In Kitaifa
SHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) Mkoa wa Dar es Salaam, limemtaka Rais John Magufuli kutupia jicho sekta binafsi.
Pia, limesema linamuunga mkono Rais kwa kuwachukulia hatua wafanyakazi wa serikali zaidi ya 9,000 walioghushi vyeti, lakini linamuomba kuwatazama kwa jicho la huruma wafanyakazi hao, ambao wamesimamishwa kazi kuanzia leo, na kuwasamehe hasa wale waliobakiza miezi michache kustaafu.
Aidha, TUCTA imeomba serikali kuanza kuwachukulia hatua viongozi wa umma wakiwemo wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya, wanaowadhalilisha wafanyakazi kwa kuwatolea lugha za matusi na wengine kuwapiga, kwani vitendo hivyo pamoja na kuwavunjia heshima wafanyakazi hao pia vinawapunguzia morali wa kuwajibika.
Hayo yalibainishwa Dar es Salaam na Mwenyekiti wa shirikisho hilo mkoa wa Dar es Salaam, George Faustine, wakati akizungumza kwenye maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi, iliyoadhimishwa jijini humo kimkoa.
Ametaja changamoto hizo kuwa ni pamoja na kutozwa kodi kubwa katika mishahara ya wafanyakazi, huku wafanyakazi hao wakiendelea kununua bidhaa ambazo pia zinatoza kodi na hivyo kuongeza mzigo wa maisha kuwa magumu kwa wafanyakazi hao.
Kwa upande wake, Mwenyekiti mstaafu wa TUCTA na Mbunge wa Urambo, Margaret Sitta ,amewataka wafanyakazi kuhakikisha wanajiunga na vyama vya wafanyakazi ili kuongeza umoja katika kudai haki zao, lakini pia kujiwekea mazingira mazuri ya kufanya kazi.
Maadhimisho hayo yalianza kwa maandamano kutoka taasisi, Kampuni na mashirika mbalimbali ,ikiwemo kutangaza bidhaa zao mbele ya wageni waliohudhuria sherehe hizo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu