Tume ya Uchaguzi na viongozi wa upinzani wakubaliana kuhusu kituo cha kujumuisha matokeo.

In Kimataifa

Muungano wa upinzani nchini Kenya NASA, umeafikiana na Tume ya Uchaguzi IEBC kuhusu utaratibu wa upinzani kuwa na kituo chao cha kujumuisha matokeo ya urais wakati wa Uchaguzi Mkuu mwezi Agosti.

Baada ya kukutana na viongozi wa Tume ya Uchaguzi jijini Nairobi, imekubaliwa kuwa upinzani unaweza kuendelea na mpango wao wa kuwa na kituo cha kujumuisha matokeo lakini usitangaze matokeo.

Mwenyekiti wa Tume hiyo Wafula Chebukati, amesema mawakala wa upinzani watakuwa na haki ya kisheria  kupata matokeo yote ya mwisho kutoka katika vituo mbalimbali lakini akasisitiza kuwa ni Tume tu ndiyo itakayokuwa na mamlaka  ya kutangaza matokeo ya mwisho.

Mwafaka huu unamaanisha kuwa, tofauti zilizokuwepo kati ya pande hizi  mbili zimetatuliwa na suluhu kupatikana.

Kigogo wa upinzani Raila Odinga na mwenzake Kalonzo Musyoka wamekuwa wakisisitiza kuwa upinzani umeweka mikakati ya kuwa na kituo chake cha kujumuisha matokeo na kuyatangaza na kusisitiza kuwa hakuna atakayewazuia kufanya hivyo.

Muungano wa NASA hivi karibuni umekuwa ukihoji utayari wa Tume ya Uchaguzi nchini humo na hata kusema hauwaamini Makamishena hao.

Hata hivyo, Tume ya Uchaguzi inasema zoezi hilo litakuwa huru na haki na ipo tayari kuandaa Uchaguzi huo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu