Tunashukuru kwa ahadi ya dola Bilioni 6 kwa Syria-O’Brien

In Kimataifa

Mkuu wa masuala ya kibinadamu wa Umoja wa mataifa Stephen O’Brien amekaribisha ahadi ya wahisani ya takribani dola bilioni 6 ili kuisaidia Syria na ukanda mzima kwa mwaka 2017 ikiwa ni ahadi kutoka kwa wahisani 41.

Dola zingine bilioni 3.7 zimeahidiwa na wahisani haohao kwa ajili ya mwaka 2018 na zaidi.

Hata hivyo wakati zahma kubwa kabisa ya kibinadamu na wakimbizi Syria ikiingia mwaka was aba , mustakhbali wa watu na taifa hilo bado uko njia panda ameonya O’Brien.

Umoja wa mataifa na washirika wake waliohudhuria mkutano wa kimataifa wa usaidizi kwa ajili ya Syria mjini Brussels Ubelgiji wanalenga kuwafikia watu milioni 12.8 mwaka huu walio ndani ya Syria na nje kama wakimbizi.

O’Brien amesema mkutano huo kwa ajili ya Syria umemalizika na nia moja ya kimataifa, kuendelea kusaidia mgogoro huo na mamilioni ya watu wanaohitaji msaada.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu