Tunashukuru kwa ahadi ya dola Bilioni 6 kwa Syria-O’Brien

In Kimataifa

Mkuu wa masuala ya kibinadamu wa Umoja wa mataifa Stephen O’Brien amekaribisha ahadi ya wahisani ya takribani dola bilioni 6 ili kuisaidia Syria na ukanda mzima kwa mwaka 2017 ikiwa ni ahadi kutoka kwa wahisani 41.

Dola zingine bilioni 3.7 zimeahidiwa na wahisani haohao kwa ajili ya mwaka 2018 na zaidi.

Hata hivyo wakati zahma kubwa kabisa ya kibinadamu na wakimbizi Syria ikiingia mwaka was aba , mustakhbali wa watu na taifa hilo bado uko njia panda ameonya O’Brien.

Umoja wa mataifa na washirika wake waliohudhuria mkutano wa kimataifa wa usaidizi kwa ajili ya Syria mjini Brussels Ubelgiji wanalenga kuwafikia watu milioni 12.8 mwaka huu walio ndani ya Syria na nje kama wakimbizi.

O’Brien amesema mkutano huo kwa ajili ya Syria umemalizika na nia moja ya kimataifa, kuendelea kusaidia mgogoro huo na mamilioni ya watu wanaohitaji msaada.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu