Watu mbalimbali wamejitokeza katika Uwanja wa Ndege wa
Kimataifa wa Julius Nyerere, kumpokea Makamu Mwenyekiti
wa CHADEMA-Bara Tundu Lissu, ambaye amerejea leo
kutokea Ubelgiji alipokwenda kwa ajili ya matibabu baada ya
kushambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana Septemba 2017
Lissu aliondoka Tanzania baada ya kushambuliwa kwa risasi
akiwa jijini Dodoma Septemba 2017 na akakimbizwa kwa
matibabu Kenya na baadaye nchini Ubelgiji alikokaa kwa
takribani miaka mitatu.