Twaweza watoa utafiti juu ya huduma za afya nchini

In Afya, Kitaifa

Kuna dalili za kupungua muda wa wagonjwa kumuona daktari, baada ya utafiti kuonyesha wale waliokuwa wakisubiri kwa zaidi ya saa moja idadi yao imeshuka kwa asilimia tano, ndani ya miaka mitatu iliyopita.

Utafiti mpya wa asasi ya kiraia ya Twaweza uliozinduliwa leo, unabainisha idadi ya wananchi wanaosubiri kumuona daktari kwa zaidi ya saa moja, imeshuka kutoka asilimia 25 mwaka 2014 hadi asilimia 20 mwaka huu.

Hii ina maana kuwa kwa sasa ni mtu mmoja kati ya watu watano wanaoenda kituo cha afya, ndio husubiri zaidi ya saa moja kupata huduma kulinganisha na mtu mmoja kati ya wanne miaka mitatu iliyopita.

Mbali na mafanikio hayo utafiti huo wa toleo la 19 la Sauti za Wananchi, unabainisha kuwa wananchi sita kati ya 10 sawa na asilimia 61, wanapata huduma za afya katika vituo vya afya vya Serikali, kiwango ambacho ni sawa na cha mwaka jana.

Mwaka 2014 idadi ya wananchi waliokuwa wakipata huduma za afya kwenye vituo vya umma, ilikuwa ni takriban watano kwa kila 10 sawa na asilimia 45.

Kutokana nay ale yalimo katika utafiti huo  mbunge wa kigoma mjini Zitto kabwe, akiongelea utafiti huo na kusema kuna umuhimu kwa kila mtanzania kuwa na bima ya afya.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu