Uchaguzi wa kenya wakumbwa na sintofahamuu.

In Kimataifa, Siasa

Nchini Kenya mjadala unaendelea kufuatia kiongozi wa upinzani Raila Odinga kujiondoa, katika kinyang’anyiro cha uchaguzi wa marudio uliopangwa kufanyika Oktoba 26.

Kumekuwa na maswali mengi kuhusu je uchaguzi utafanyika au mgombea aliyebaki Rais Uhuru Kenyatta, atangazwe kuwa mshindi bila kufanyika uchaguzi.

Tayari Rais Uhuru Kenyatta amesema pamoja na kujiondoa Raila Odinga wa NASA uchaguzi utafanyika kama ulivyopangwa.

Katika kupata ufafanuzi zaidi kuhusu utata huo Antenna imemnasa Mwandishi wetu Dkt Alutalala Mukhwana, ambaye ni mwanasheria aliyebobea katika masuala ya Kikatiba nchini humo.

Kwa upande wake Rais uhuru Kenyeta hakukaa kimya baada ya Raila Odinga kutangaza kujitoa katika uchaguzi huo, ni lipi alilolisema msikie hapa.

Hata hivyo habari nyingine ni kwamba, mahakama Kuu nchini humo imeamuru mgombea urais wa chama cha Thirdway Alliance Ekuru Aukot, aliyekuwa ameshiriki uchaguzi mkuu tarehe 8 Agosti, ashirikishwe kwenye uchaguzi mkuu mpya unaopangiwa kufanyika tarehe 26 Oktoba.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu