#UEFAChampionsLeague: Klabu za EPL na La Liga zatawala 16 bora

In Kimataifa, Michezo

Michuano ya klabu bingwa barani Ulaya hatua ya makundi imemalizika jana ambapo tayari timu 16 kati ya 32 zimefanikiwa kutinga hatua ya 16 bora, hatua ya mtoano.

Kwenye hatua hiyo klabu za kutoka Ligi Kuu Uingereza  na zile kutoka La Liga ndio zimetawala 16 bora ya michuano hiyo, ambapo Uingereza imeingiza timu zote tano huku Hispania ikifanikiwa kuingiza timu tatu.

Timu zilizofanikiwa kupita kutoka Uingereza ni Liverpool, Manchester United, Manchester City, Tottenham Hotspurs na Chelsea.

Na timu zilizofuzu kutoka Uhispania ni Real Madrid, Barcelona na Sevilla huku klabu ya Atletico Madrid ikitolewa mapema kwenye michuano hiyo.

Kwa upande mwingine timu 16 ambazo  zimetolewa kwenye michuano hiyo zitaingia moja kwa moja kwenye hatua ya makundi ya michuano ya Europa.

Droo ya kutangaza ratiba ya hatua ya 16 bora ya kombe la klabu bingwa barani Ulaya itafanyika jumatatu ya tarehe 11 Desemba 2017, huko mjini Nyon , Uswizi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu