#UEFAChampionsLeague: Klabu za EPL na La Liga zatawala 16 bora

In Kimataifa, Michezo

Michuano ya klabu bingwa barani Ulaya hatua ya makundi imemalizika jana ambapo tayari timu 16 kati ya 32 zimefanikiwa kutinga hatua ya 16 bora, hatua ya mtoano.

Kwenye hatua hiyo klabu za kutoka Ligi Kuu Uingereza  na zile kutoka La Liga ndio zimetawala 16 bora ya michuano hiyo, ambapo Uingereza imeingiza timu zote tano huku Hispania ikifanikiwa kuingiza timu tatu.

Timu zilizofanikiwa kupita kutoka Uingereza ni Liverpool, Manchester United, Manchester City, Tottenham Hotspurs na Chelsea.

Na timu zilizofuzu kutoka Uhispania ni Real Madrid, Barcelona na Sevilla huku klabu ya Atletico Madrid ikitolewa mapema kwenye michuano hiyo.

Kwa upande mwingine timu 16 ambazo  zimetolewa kwenye michuano hiyo zitaingia moja kwa moja kwenye hatua ya makundi ya michuano ya Europa.

Droo ya kutangaza ratiba ya hatua ya 16 bora ya kombe la klabu bingwa barani Ulaya itafanyika jumatatu ya tarehe 11 Desemba 2017, huko mjini Nyon , Uswizi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu