Ufaransa hivi majuzi ulipata pigo la kupata Visa baada ya mamlaka ya Rwanda kukataa ombi lao

In Kimataifa

Ujumbe wa kidiplomasia wa taifa la Ufaransa hivi majuzi ulipata pigo la kupata Visa baada ya mamlaka ya Rwanda kukataa ombi lao walilowasilisha ambalo lilishirikisha picha ya bendera ya zamani ya taifa hilo ambayo ilitumika wakati wa mauaji ya halakiki ya 1994 kulingana na ripoti za jarida la Jeune Afrique.

Gazeti hilo limeelezea hatua hiyo kama vuta ni kuvute ya kwanza katika uhusiano kati ya utawala huo mpya wa Ufaransa na Kigali.

Linasema kuwa mnamo terehe 9 na 10 ujumbe rasmi wa Ufaransa ulitarajiwa kusafiri kuelekea Cameroon kupitia Kigali .

Ujumbe huo ulishirikisha Mkurugenzi wa eneo la Afrika na bahari Hindi katika wizara ya maswala ya kigeni ,mkurugenzi wa eneo la jangwa la Sahara chini ya idara ya maendeleo nchini Ufaransa pamoja na mshauri wa kiuchumi ambao walitarajiwa kukutana na waziri wa mswala ya kigeni nchini Rwanda Luoise Mushikwabo mjini Kigali.

Mapema mwezi Julai, waziri wa maswala ya kigeni nchini Ufaransa aliwasilisha ombi la Visa kwa ubalozi wa Rwanda mjini Paris pamoja na ujumbe wao.

Katika kila taifa walilotembea kulikuwa na picha ya bendera.

Bendera ya Rwanda iliochapishwa ilikuwa kamili na rangi tatu za kijani, manjano na nyekundu ikiwa na herufi kubwa ya R katikati.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu