Gazeti hilo limeelezea hatua hiyo kama vuta ni kuvute ya kwanza katika uhusiano kati ya utawala huo mpya wa Ufaransa na Kigali.
Linasema kuwa mnamo terehe 9 na 10 ujumbe rasmi wa Ufaransa ulitarajiwa kusafiri kuelekea Cameroon kupitia Kigali .
Ujumbe huo ulishirikisha Mkurugenzi wa eneo la Afrika na bahari Hindi katika wizara ya maswala ya kigeni ,mkurugenzi wa eneo la jangwa la Sahara chini ya idara ya maendeleo nchini Ufaransa pamoja na mshauri wa kiuchumi ambao walitarajiwa kukutana na waziri wa mswala ya kigeni nchini Rwanda Luoise Mushikwabo mjini Kigali.
Mapema mwezi Julai, waziri wa maswala ya kigeni nchini Ufaransa aliwasilisha ombi la Visa kwa ubalozi wa Rwanda mjini Paris pamoja na ujumbe wao.
Katika kila taifa walilotembea kulikuwa na picha ya bendera.
Bendera ya Rwanda iliochapishwa ilikuwa kamili na rangi tatu za kijani, manjano na nyekundu ikiwa na herufi kubwa ya R katikati.
