Ufaransa yazindua mipango ya kuanzisha vituo vya kusajili wahamiaji.

In Kimataifa

Ufaransa imezindua mipango ya kuanzisha vituo vya kusajili wahamiaji wanaotafuta hifadhi huko nchini Libya, huku bara la Ulaya likiwa linakabiliwa na wimbi la wahamiaji wanaovuka bahari ya Mediterenia.

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amesema mpango huo utaanza rasmi msimu huu wa joto na utawapa fursa wahamiaji kutafuta hifadhi wakiwa barani Afrika.

Libya imekuwa kituo kikuu kwa wahamiaji wa Kiafrika wanaojaribu kuingia barani Ulaya kwa kutumia boti dhaifu ambazo mara kwa mara kuzama na zinazoendeshwa na wafanya biashara haramu.

Libya inajaribu kuzuia safari hizo haramu huku yenyewe ikiwa inapambana na ombwe la kitawala na kisiasa tangu kupinduliwa na kuuwawa kwa kiongozi wa zamani na wa muda mrefu Muamar Gaddafi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu