Ufaransa yazindua mipango ya kuanzisha vituo vya kusajili wahamiaji.

In Kimataifa

Ufaransa imezindua mipango ya kuanzisha vituo vya kusajili wahamiaji wanaotafuta hifadhi huko nchini Libya, huku bara la Ulaya likiwa linakabiliwa na wimbi la wahamiaji wanaovuka bahari ya Mediterenia.

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amesema mpango huo utaanza rasmi msimu huu wa joto na utawapa fursa wahamiaji kutafuta hifadhi wakiwa barani Afrika.

Libya imekuwa kituo kikuu kwa wahamiaji wa Kiafrika wanaojaribu kuingia barani Ulaya kwa kutumia boti dhaifu ambazo mara kwa mara kuzama na zinazoendeshwa na wafanya biashara haramu.

Libya inajaribu kuzuia safari hizo haramu huku yenyewe ikiwa inapambana na ombwe la kitawala na kisiasa tangu kupinduliwa na kuuwawa kwa kiongozi wa zamani na wa muda mrefu Muamar Gaddafi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu