Ujerumani na China zimeitolea mwito Marekani isiutupilie mbali mkataba wa mabadiliko ya tabia ya nchi ulioafikiwa mjini Paris nchini Ufaransa.

In Kimataifa

Ujerumani na China zimeitolea mwito Marekani isiutupilie mbali mkataba wa mabadiliko ya tabia ya nchi ulioafikiwa mjini Paris nchini Ufaransa.

Mwito huo umetolewa kwenye mkutano uliofanyika katika mji mkuu wa Ujerumani, Berlin.

Rais wa Marekani Donald Trump amewahi kusema Marekani itajiondoa kutoka kwa mkataba huo baada ya kusema mabadiliko ya tabia nchi ni uongo.

Ujerumani na China zimeitaka Marekani iuheushimu mkataba huo wa Paris huku Marekani ikijiandaa kuamua mustakabali wake kuhusu mkataba huo.

Katika taarifa ya pamoja mwanzoni mwa Mdahalo kuhusu hali ya hewa huko Petersburg, Berlin, mawaziri wa mazingira wa Ujerumani na China wameitaka Marekani isijiondoe kutoka mkataba wa Paris.

Waziri wa mazingira wa Ujerumani Barbara Hendricks amesema wanawasiliana na maafisa wa ngazi zote za Marekani kuwashawishi wabakie katika mkataba huo.

Hendricks amesema anaamini kubakia kwa Marekani kutaimarisha juhudi za kupunguza ongezeko la joto na huenda kutainufaisha zaidi Marekani kiuchumi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu