Ujerumani na China zimeitolea mwito Marekani isiutupilie mbali mkataba wa mabadiliko ya tabia ya nchi ulioafikiwa mjini Paris nchini Ufaransa.

In Kimataifa

Ujerumani na China zimeitolea mwito Marekani isiutupilie mbali mkataba wa mabadiliko ya tabia ya nchi ulioafikiwa mjini Paris nchini Ufaransa.

Mwito huo umetolewa kwenye mkutano uliofanyika katika mji mkuu wa Ujerumani, Berlin.

Rais wa Marekani Donald Trump amewahi kusema Marekani itajiondoa kutoka kwa mkataba huo baada ya kusema mabadiliko ya tabia nchi ni uongo.

Ujerumani na China zimeitaka Marekani iuheushimu mkataba huo wa Paris huku Marekani ikijiandaa kuamua mustakabali wake kuhusu mkataba huo.

Katika taarifa ya pamoja mwanzoni mwa Mdahalo kuhusu hali ya hewa huko Petersburg, Berlin, mawaziri wa mazingira wa Ujerumani na China wameitaka Marekani isijiondoe kutoka mkataba wa Paris.

Waziri wa mazingira wa Ujerumani Barbara Hendricks amesema wanawasiliana na maafisa wa ngazi zote za Marekani kuwashawishi wabakie katika mkataba huo.

Hendricks amesema anaamini kubakia kwa Marekani kutaimarisha juhudi za kupunguza ongezeko la joto na huenda kutainufaisha zaidi Marekani kiuchumi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu