Umoja wa makanisa nchini kufanya maombi ya shukrani kitaifa.

In Kitaifa

Umoja wa makanisa mbalimbali nchini, unatarajia kufanya maombi ya shukrani kitaifa ya saa tano Jumamosi ijayo.

Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya maombi hayo, Askofu Dk David Mwasota amesema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maandalizi yake jijini Dar es Salaam.

Askofu huyo amesema maombi hayo ni kwa ajili ya kumshukuru Mungu, kwa kuwawezesha kumpata Rais John Magufuli, ambaye amekuwa akiibua na kufichua maovu mbalimbali yaliyokuwa yakitendeka nchini.

Aidha, amesema maombi hayo ni mwitikio wa Rais Magufuli, ambaye mara nyingi amekuwa akisema anahitaji watanzania wamuombee ambapo yatafanyika  Julai 15, mwaka huu katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam kuanzia saa 3 asubuhi hadi saa 8 mchana.

Amesema katika maombi hayo, wanategemea kupata ugeni wa maaskofu 17 kutoka Marekani, umoja wa maaskofu wa makanisa Afrika Kusini watakuwepo wajumbe 41 na wajumbe mbalimbali kutoka mikoani hapa nchini ambapo ametoa  mwito kwa wakazi wa Dar es Salaam na mikoa jirani, kufika Uwanja wa Uhuru kushiriki.

 

 

 

 

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Serikali kuunga mkono juhudi za Taasisi mbali mbali.

Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Mwinyi, amesema serikaliitaendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Taasisi yaZanzibar Maisha Bora Foundation,pamoja na

Read More...

DKT. KIRUSWA AZINDUA MFUMO WA USHIRIKISHWAJI WA WATANZANIA KATIKA SEKTA YA MADINI

Watanzania waendelea kunufaika Sekta ya Madini, ajira 15,341 zamwagwa, manunuzi ya ndani ya nchi yafikia Dola za Marekani bilioni

Read More...

MAFURIKO YAUWA 190 MALAWI

Takriban watu 190 sasa wamethibitishwa kufariki nchini Malawi baada ya Dhoruba ya Mafuriko ya Tropiki Freddy kulikumba eneo

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu