Umoja wa makanisa nchini kufanya maombi ya shukrani kitaifa.

In Kitaifa

Umoja wa makanisa mbalimbali nchini, unatarajia kufanya maombi ya shukrani kitaifa ya saa tano Jumamosi ijayo.

Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya maombi hayo, Askofu Dk David Mwasota amesema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maandalizi yake jijini Dar es Salaam.

Askofu huyo amesema maombi hayo ni kwa ajili ya kumshukuru Mungu, kwa kuwawezesha kumpata Rais John Magufuli, ambaye amekuwa akiibua na kufichua maovu mbalimbali yaliyokuwa yakitendeka nchini.

Aidha, amesema maombi hayo ni mwitikio wa Rais Magufuli, ambaye mara nyingi amekuwa akisema anahitaji watanzania wamuombee ambapo yatafanyika  Julai 15, mwaka huu katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam kuanzia saa 3 asubuhi hadi saa 8 mchana.

Amesema katika maombi hayo, wanategemea kupata ugeni wa maaskofu 17 kutoka Marekani, umoja wa maaskofu wa makanisa Afrika Kusini watakuwepo wajumbe 41 na wajumbe mbalimbali kutoka mikoani hapa nchini ambapo ametoa  mwito kwa wakazi wa Dar es Salaam na mikoa jirani, kufika Uwanja wa Uhuru kushiriki.

 

 

 

 

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu