Umoja wa Mataifa umegundua Umoja wa makaburi zaidi ya 38 katika jimbo la kati la Kasai.

In Kimataifa

Umoja wa Mataifa umegundua kile kinachoonekana kuwa ni makaburi zaidi ya pamoja 38 katika jimbo la kati la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo linalokumbwa na machafuko la Kasai.

Mkurugenzi wa Ofisi ya Pamoja ya Haki za Binaadamu ya Umoja wa Mataifa nchini Congo Jose Maria Aranaz amewaambia waandishi wa habari mjini Kinshasa kuwa makaburi hayo mapya 38 yanajumuisha 31 katika eneo la Diboko, na saba katika eneo la Sumbula, upande wa magharibi mwa Kasai.

Yaligunduliwa kufuatia uchunguzi wa pamoja wa Umoja wa Mataifa na idara ya mahakama ya jeshi la Congo kati ya Julai 4 na 7.

Ugunduzi huo unafikisha 90, jumla ya makaburi ya pamoja yaliyotangazwa na Umoja wa Mataifa au maafisa wa Congo katika mkoa huo.

Mzozo wa Kasai ulichochewa na kukataa kwa serikali kumpa utambulisho rasmi Jean-Pierre Mpandi, anayefahamika kama Kamuina Nsapu, kuwa mmoja wa viongozi wa kitamaduni wa eneo hilo.

Mpandi kisha akawatumia wapiganaji wake kuanzisha uasi dhidi ya uwepo wa serikali katika eneo hilo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu