Umoja wa Mataifa umesema wanajeshi wa serikali nchini Sudan Kusini, wamewauawa raia 114 katika mji wa Yei kati ya mwezi Julai mwaka 2016 na Januari mwaka 2017.

In Kimataifa

Umoja wa Mataifa umesema wanajeshi wa serikali nchini Sudan Kusini, wamewauawa raia 114 katika mji wa Yei kati ya mwezi Julai mwaka 2016 na Januari mwaka 2017.

Mbali na mauaji hayo, Tume inayoshughulikia maswala ya haki za Binadamu katika Umoja huo imesema  wanawake na wasichana wamebakwa lakini pia mali kuibiwa mali zao na kuteswa.

Watalaam wa Umoja wa Mataifa waliofanya uchunguzi katika mji huo wanasema, mauaji haya yaliegemea ukabila, na yamekuwa mabaya sana kuwahi kutekelezwa na jeshi la serikali katika siku za hivi karibuni.

Hata hivyo, msemaji wa jeshi Kanali Santo Domic Chol ameliambia Shirika la Habari la Uingereza la Reuters kuwa ripoti hiyo ya Umoja wa Mataifa sio ya kweli.

Ameongeza kuwa hii sio mara ya kwanza kwa Umoja wa Mataifa kuishutumu jeshi la nchi yake kwa lengo la kuichafulia jina na kulifanya lionekane ni maadui wa raia wake.

Ripoti hii imekuja baaada ya rais Salva Kiir kumfuta kazi aliyekuwa Mkuu wa majeshi Paul  Malong.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

ZOEZI LA UOKOAJI HANANG, MAWAZIRI WAFIKA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista J. Mhagama, Waziri wa Ujenzi Innocent

Read More...

RC MBEYA AFANYA UZINDUZI ZOEZI LA UGAWAJI VITAMBULISHO VYA (NIDA)

Mkuu wa mkoa wa mbeya Mhe. Comrede Juma Zuberi Homera amefanya uzinduzi wa wa zoezi la ugawaji wa vitambulisho

Read More...

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu