Umoja wa Mataifa umetoa wito wa kusitishwa kwa muda mapigano.

In Kimataifa

Umoja wa Mataifa umetoa wito wa kusitishwa kwa muda mapigano ili kuruhusu kiasi ya raia 20,000 waliozingirwa kwenye mji wa Raqqa, nchini Syria, waweze kuondoka.

Umoja huo pia umevitaka vikosi vinavyoongozwa na Marekani kusitisha mashambulizi ya anga ambayo yamesababisha majeruhi.

Mshauri wa masuala ya kiutu wa Umoja wa Mataifa nchini Syria, Jan Egeland amewaambia waandishi habari mjini Geneva, Uswisi, kwamba boti katika Mto Euphrates hazipaswi kushambuliwa na kwamba watu wanaotoka kwenye boti hizo hawawezi kuhatarisha maisha yao kwa mashambulizi ya anga.

Aidha, mjumbe msaidizi wa Umoja wa Mataifa nchini Syria, Ramzy Ezzeldin, amesema umoja huo bado unatathmini matokeo ya mazungumzo yaliyofanyika wiki hii mjini Riyadh kati ya makundi matatu ya upinzani ya Syria ambayo yalishindwa kuungana.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu