Uongozi wa shule za msingi ukombozi na Engosengiu waishukuru halimashauri ya Jiji la Arusha kwa kuweza kutatua changamoto zilizokua zikiwakabili.

In Kitaifa

Uongozi na wanafunzi wa shule za msingi ukombozi na Ongosengiu zilizopo kata ya sinoni mkoani Arusha, zimeishukuru halmashauri  ya jiji kwa kuweza kutatua changamoto zilizokuwa zikiwakabili, kwa mda mrefu katika shule hizo

Wakizungumza baada ya kutembelewa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo ,katika ziara ya kikazi ya kukagua miradi ya maendeleo na kutatua kero zinazowakabili wananchi baadhi ya waalimu wamesema wamekuwa wakikabiliwa na changamoto ya vyoo, na madarasa hali ambayo inawapelekea kuwa na wasiwasi wa magonjwa ya milipuko kama kipindupindu

Aidha kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amekabithi jumla ya madarasa 17 ,katika shule hizo huku akiahidi kujenga vyoo na kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili waalimu wa shule hizo

Hata hivyo amewataka waalimu wa shule za msingi na sekondari kufanya kazi kwa ufanisi ,ikiwa ni pamoja na kuwafundisha wanafunzi kwa bidii ili kuweza kujenga Tanzania ya viwanda ambayo Ndio azma ya Seriakali ya Awamu ya Tano .

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

ZOEZI LA UOKOAJI HANANG, MAWAZIRI WAFIKA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista J. Mhagama, Waziri wa Ujenzi Innocent

Read More...

RC MBEYA AFANYA UZINDUZI ZOEZI LA UGAWAJI VITAMBULISHO VYA (NIDA)

Mkuu wa mkoa wa mbeya Mhe. Comrede Juma Zuberi Homera amefanya uzinduzi wa wa zoezi la ugawaji wa vitambulisho

Read More...

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu