Upinzani Afrika kusini wataka Bunge livunjwe.

In Kimataifa

Chama kikuu cha upinzani nchini Afrika Kusini hapo jana kiliwasilisha hoja kikitaka bunge la nchi hiyo livunjwe na uchaguzi uitishwe mapema, ikiwa ni siku chache baada ya hoja ya kupiga kura ya kutokuwa na imani na Rais Jacob Zuma kugonga mwamba.

Graham Charters, msemaji wa chama cha upinzani cha Democratic Alliance, amesema hoja hiyo mpya tayari imewasilishwa kwa spika wa bunge atakayeamua iwapo itapelekwa mbele ya bunge.

Zuma, mwenye umri wa miaka 75 ambaye kipindi chake cha pili na cha mwisho cha uongozi kinamalizika mwaka 2019, amenusurika mara kadhaa kuondolewa madarakani kupitia kura ya kutokuwa na imani naye iliyoitishwa kufuatia tuhuma za rushwa na matumizi mabaya ya madaraka.

Hata hivyo, chama cha ANC hapo jana kiliapa kuikwamisha hoja hiyo kama kilivyowahi kukwamisha hoja nyingine kama hizo zenye lengo la kuiangusha serikali ya chama hicho.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu