Upinzani Afrika kusini wataka Bunge livunjwe.

In Kimataifa

Chama kikuu cha upinzani nchini Afrika Kusini hapo jana kiliwasilisha hoja kikitaka bunge la nchi hiyo livunjwe na uchaguzi uitishwe mapema, ikiwa ni siku chache baada ya hoja ya kupiga kura ya kutokuwa na imani na Rais Jacob Zuma kugonga mwamba.

Graham Charters, msemaji wa chama cha upinzani cha Democratic Alliance, amesema hoja hiyo mpya tayari imewasilishwa kwa spika wa bunge atakayeamua iwapo itapelekwa mbele ya bunge.

Zuma, mwenye umri wa miaka 75 ambaye kipindi chake cha pili na cha mwisho cha uongozi kinamalizika mwaka 2019, amenusurika mara kadhaa kuondolewa madarakani kupitia kura ya kutokuwa na imani naye iliyoitishwa kufuatia tuhuma za rushwa na matumizi mabaya ya madaraka.

Hata hivyo, chama cha ANC hapo jana kiliapa kuikwamisha hoja hiyo kama kilivyowahi kukwamisha hoja nyingine kama hizo zenye lengo la kuiangusha serikali ya chama hicho.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Serikali kuunga mkono juhudi za Taasisi mbali mbali.

Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Mwinyi, amesema serikaliitaendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Taasisi yaZanzibar Maisha Bora Foundation,pamoja na

Read More...

DKT. KIRUSWA AZINDUA MFUMO WA USHIRIKISHWAJI WA WATANZANIA KATIKA SEKTA YA MADINI

Watanzania waendelea kunufaika Sekta ya Madini, ajira 15,341 zamwagwa, manunuzi ya ndani ya nchi yafikia Dola za Marekani bilioni

Read More...

MAFURIKO YAUWA 190 MALAWI

Takriban watu 190 sasa wamethibitishwa kufariki nchini Malawi baada ya Dhoruba ya Mafuriko ya Tropiki Freddy kulikumba eneo

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu