Upo uwezekano wa wanyama kama mbwa mwitu, tembo, sokwe na faru mweusi kutoweka.

In Kitaifa

Mamlaka ya Hifadhi za Taifa(TANAPA), imesema iwapo watanzania hususani wanaoishi karibu na hifadhi za taifa na mbuga za wanyama hawatakuwa walinzi wa rasilimali za taifa, upo uwezekano wa wanyama kama mbwa mwitu, tembo, sokwe na faru mweusi wakatoweka.

Kutokana na hali hiyo, huenda wanyama hao wakaonekana zaidi kupitia picha za video na za mnato, na kutaka kila mwananchi kuwa mlinzi wa rasilimali hizo kwa kuwataja majangili wanaojihusisha na uwindaji harama wa wanyama hao.

Mkurugenzi Mkuu wa Tanapa, Allan Kijazi amesema hayo wakati akifungua warsha ya siku tatu ya waandishi wa habari mkoani Kilimanjaro, iliyoandaliwa na chama cha wanahabari mkoani hapa (Mecki) na kuratibiwa na hifadhi ya taifa ya mlima Kilimanjaro (KINAPA) na kufanyika mjini Moshi.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi mkuu, Mkurugenzi wa uhifadhi wa Tanapa, Mtango Mtahiko, amesema Tanzania ni moja ya nchi zenye sifa ya uhifadhi wenye uoto wa asili jambo ambalo limekuwa likivuta idadi kubwa ya watalii kutoka nchi mbalimbali duniani.

 

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu