Urusi na Belarus zimeanza mazoezi makubwa ya pamoja ya kijeshi.

In Kimataifa

Urusi na Belarus zimeanza mazoezi makubwa ya pamoja ya kijeshi, ambayo yamepewa jina Zapad-2017, ambayo yamezitia wasiwasi nchi jirani na wanachama wa shirika la kujihami la nchi za Magharibi la Nato.

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Urusi imesema kuwa wanajeshi 12,700 wanashiriki mazoezi hayo, lakini wataalamu wa Nato wamesema kuwa idadi inaweza ikawa iko juu zaidi ya hiyo.

Aidha Rais wa Ukraine, Petro Poroshenko ameonya kuwa Zapad-2017 jina ambalo maana yake kwa Kirusi ni “Magharibi” huenda ikawa ni hatua ya mwisho kabla ya kuivamia Ukraine.

Hata hivyo, Makundi ya wapiganaji wanaoungwa mkono na Urusi tayari wanayashikilia maeneo makubwa ya mashariki mwa Ukraine na wameendelea kukabiliana na wanajeshi wa nchi hiyo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu