Urusi na Belarus zimeanza mazoezi makubwa ya pamoja ya kijeshi.

In Kimataifa

Urusi na Belarus zimeanza mazoezi makubwa ya pamoja ya kijeshi, ambayo yamepewa jina Zapad-2017, ambayo yamezitia wasiwasi nchi jirani na wanachama wa shirika la kujihami la nchi za Magharibi la Nato.

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Urusi imesema kuwa wanajeshi 12,700 wanashiriki mazoezi hayo, lakini wataalamu wa Nato wamesema kuwa idadi inaweza ikawa iko juu zaidi ya hiyo.

Aidha Rais wa Ukraine, Petro Poroshenko ameonya kuwa Zapad-2017 jina ambalo maana yake kwa Kirusi ni “Magharibi” huenda ikawa ni hatua ya mwisho kabla ya kuivamia Ukraine.

Hata hivyo, Makundi ya wapiganaji wanaoungwa mkono na Urusi tayari wanayashikilia maeneo makubwa ya mashariki mwa Ukraine na wameendelea kukabiliana na wanajeshi wa nchi hiyo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu