Uturuki leo inaadhimisha mwaka mmoja tangu jaribio la kuipindua serikali ya Rais Recep Tayyip Erdogan.

In Kimataifa

Uturuki leo inaadhimisha mwaka mmoja tangu jaribio la kuipindua serikali ya Rais Recep Tayyip Erdogan mara baada ya kushindwa kufanya mapinduzi hayo.

Tangu jaribio hilo, serikali imeendelea kuwakamata maelfu ya watu wakiwemo wanahabari na kuwafuta kazi maelfu ya wafanyakazi wa umma, maafisa wa usalama, wanajeshi na wasomi.

Serikali itaadhimisha tukio hilo kwa hafla mbali mbali ikiwemo hotuba tatu zitakazotolewa leo na Rais Erdogan katika miji ya Istanbul na Ankara.

Baada ya jaribio hilo la kuipindua serikali ambalo mamia ya watu walikufa, serikali ilitangaza hali ya hatari. Zaidi ya watu 50,000 wako jela kwa kushukiwa kuwa na uhusiano na hasimu mkubwa wa Erdogan, Fethullah Gulen anayeishi uhamishoni Marekani.

Serikali inamtuhumu kwa kupanga mapinduzi hayo, madai ambayo Gulen ameyakanusha.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu