Vijana sita wa timu ya Burundi ya ubunifu wa Maroboti watoweka.

In Kimataifa
Vijana sita wa timu ya Burundi ya ubunifu wa Maroboti wameripotiwa kutoweka baada ya kushiriki katika mashindano ya kimataifa nchini Marekani.
Polisi imesema wawili kati ya vijana hao waliripotiwa kuonekana wakivuka mpaka wa Marekani kuingia Canada na kuongeza kuwa hakuna “dalili zozote za kutokea uhalifu”.
Hata hivyo Shirika la Huduma za Mpakani nchini Canada, limesema haliwezi kuthibitisha wala kukanusha kuwa vijana hao wawili waliingia Canada.
Wavulana hao wanne na wasichana wawili walionekana mara ya mwisho siku ya Jumanne mchana wakati mashindano hayo ya maroboti yalipokamilika mjini Washington.
Burundi kwa muda mrefu imekumbwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe na machafuko, na kuongezeka kwa mapigano kumewalazimu watu  laki  nne ,kuyakimbia makazi yao tangu Aprili 2015, wakati Rais Pierre Nkurunziza aliposema atagombea muhula wa tatu.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu