Vijana sita wa timu ya Burundi ya ubunifu wa Maroboti watoweka.

In Kimataifa
Vijana sita wa timu ya Burundi ya ubunifu wa Maroboti wameripotiwa kutoweka baada ya kushiriki katika mashindano ya kimataifa nchini Marekani.
Polisi imesema wawili kati ya vijana hao waliripotiwa kuonekana wakivuka mpaka wa Marekani kuingia Canada na kuongeza kuwa hakuna “dalili zozote za kutokea uhalifu”.
Hata hivyo Shirika la Huduma za Mpakani nchini Canada, limesema haliwezi kuthibitisha wala kukanusha kuwa vijana hao wawili waliingia Canada.
Wavulana hao wanne na wasichana wawili walionekana mara ya mwisho siku ya Jumanne mchana wakati mashindano hayo ya maroboti yalipokamilika mjini Washington.
Burundi kwa muda mrefu imekumbwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe na machafuko, na kuongezeka kwa mapigano kumewalazimu watu  laki  nne ,kuyakimbia makazi yao tangu Aprili 2015, wakati Rais Pierre Nkurunziza aliposema atagombea muhula wa tatu.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu