Vijana wasema Jenerali wa jeshi hana nguvu zozote Zimbabwe.

In Kimataifa

Vugu vugu la vijana wa chama tawala cha Zimbabwe limemkosoa jenerali wa jeshi mwenye cheo cha juu zaidi nchini humo kufuatia kauli aliyoitoa kwamba jeshi linajiandaa kuingilia kati kumaliza mzozo wa ndani wa chama tawala cha Zanu-Pf..

Ameambia vyombo vya habari mjini Harare kwamba mkuu huyo wa jeshi haungwi mkono na jeshi lote.

Tayari chama cha upinzani nchini Zimbabwe MDC kimepuuzilia mbali kauli hiyo ya jenerali wa jeshi kikimtaja kuwa asiye na nguvu zozote.

Matamshi hayo yanajiri kufuatia hatua ya Chimwenga kutishia kufanya mapinduzi iwapo chama cha Zanu-PF hakitasita kuwafurusha wapiganaji wa uhuru katika chama hicho ambao wametofautiana na rais Robert Mugabe na mkewe Grace Mugabe.

Msemaji wa MDC Kuraoune Chihwaye alinukuliwa akisema:

”Hana nguvu zozote kumzuia Grace kuwatukana wapiganaji wa uhuru wa zamani”.

Jumatatu, jeneral Constantino Chiwenga alisema kuwa mvutano juu ya askari wa zamani lazima usitishwe.

Kauli hiyo ilipokelewa na wengi kama iliyomlenga Emmerson Mnangagwa, ambaye alifutwa kazi kama makamu wa rais wa Zimbabwe wiki iliyopita .

Taarifa zilizotolewa kwenye mitandao ya kijamii ya habari zinaelezea kuwa magari ya kivita yalionekana yakielekea katika mji mkuu Harare.

Sasa inadhaniwa kuwa ni magari ya kivita yanayosafiri kutoka kwenye kambi za kijeshi kuelekea kwenye kambi ya walinzi wa rais nje ya mji mkuu.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

NACTIVET YASIMAMISHA MAFUNZO CHUO CHA MBEYA TRAINING..DC MALISA AAGIZA KUFANYIWA UHAKIKI VYUO VYOTE WILAYA YA MBEYA

Wazazi Wanafunzi na wahitimu wa chuo cha Mbeya training wameiomba serikali iwasaidie kurudishiwa stahiki zao mara baada ya kubainika

Read More...

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMANNE NOVEMBA 7, 2023

Manchester United na Newcastle United zote zinamfuatilia mshambuliaji wa Lyon Mfaransa Rayan Cherki, 20, ambaye mkataba wake unamalizika Juni

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu