Viongozi wa dini wapenda sadaka waonywa.

In Kitaifa

Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania, limekemea baadhi ya viongozi wa kidini wanaojipendekeza kwa watu wenye fedha, kwa kutaka kuwaombea ili wapate sadaka nono.

Aidha kanisa hilo limeungana na makanisa ya Uamsho ya Moravian Marekani na duniani kote, kutoa tamko rasmi la kupinga ushoga na usagaji, na kuweka bayana kuwa halitafungisha ndoa za jinsi moja.

Askofu Mkuu wa kanisa hilo Tanzania Emmaus Mwamakula, ameyasema hayo hivi karibuni katika Ibada ya kuwasimika wachungaji, mashemasi na makasisi wa kanisa hilo iliyofanyika katika kanisa la Mbweni Dayosisi Kuu ya Dar es Salaam.

Akizungumza katika ibada hiyo Askofu Mwamakula amesema kuwa, utumishi wa Mungu katika dunia hii umewekwa kwa kusudi la kuleta amani, furaha na umoja katika jamii.

Pia kusaidia waliotindikiwa imani kumkaribia Mungu zaidi na si kujinufaisha wenyewe.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

ZOEZI LA UOKOAJI HANANG, MAWAZIRI WAFIKA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista J. Mhagama, Waziri wa Ujenzi Innocent

Read More...

RC MBEYA AFANYA UZINDUZI ZOEZI LA UGAWAJI VITAMBULISHO VYA (NIDA)

Mkuu wa mkoa wa mbeya Mhe. Comrede Juma Zuberi Homera amefanya uzinduzi wa wa zoezi la ugawaji wa vitambulisho

Read More...

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu