Viongozi wa Mamlaka ya hali ya hewa watembelea kituo cha Radio5fm

In Kitaifa

Viongozi wa Mamlaka ya hali ya hewa leo wametembelea ofisi za kituo cha Radio 5 Arusha na kujionea jinsi wanavyorusha matangazo yao.

Wakizungumza na baadhi ya watangazaji wa Radio 5, Bi Juwairia Mshana ambaye ni Meneja wa Mamlaka hiyo kanda ya Kaskazini amewashukuru Radio 5 kwa kuendelea kutoa taarifa za hali ya hewa katika vipindi vyao.

Kwa Upande wake Bw Charles Nsalamba ambae ni Meneja wa Mamlaka hiyo (TMA) mkoa wa Arusha amesema wadau mbalimbali wanapaswa kupata taarifa za hali ya hewa hivyo ni vyema kupata taarifa sahihi kutoka katika Mamlaka ya hali ya hewa Tanzania (TMA).

Muwakilishi toka Uk Met ya nchini Uingereza ameipongeza Radio 5 kwa kuendelea kuwapa taarifa wananchi juu ya utabiri wa hali ya hewa.

 

 

Akizungumza mbele ya wageni hao kiongozi wa kipindi cha Kilimo Radio 5 Hilda Kinabo amewashukuru mamlaka hiyo kwa kuendelea kuwa karibu na Radio 5 hususani katika kutoa taarifa za hali ya hewa jambo linalo wasaidia kufikisha ujumbe kwa wakulima wanaotegemea Radio 5 kupata taarifa za hali ya hewa.

0

Kwa niaba ya Uongozi wa Radio 5 msimamizi wa vipindi wa kituo cha Radio 5 Bw Semio Sonyo amewashukuru viongozi wa TMA Mkoa na wa Kanda ya kaskazini pamoja na mgeni toka nchini Uingereza kwa kujali kile kinacho fanyika Radio 5 na kuwaomba waendelee kushirikiana na kituo chao katika kuhakikisha jamii inapata taarifa sahihi toka Mamlaka ya hali ya hewa Tanzania.

Radio 5 Arusha inarusha Matangazo ya hali ya hewa katika vipindi vyake kama Antenna,Fahari Yangu na vinginevyo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu