Vituo vya serikali vimekuwa vikicheza nyimbo za vita vya uhuru Zimbabwe

In Kimataifa

Vyombo vya habari vya serikali vimekuwa vikicheza nyimbo za uhuru za kuanzia wakati wa uhuru miaka ya themanini na kurudia matangazo ya Meja Jenerali Sibusiso Moyo.

Jenerali Moyo alitangaza kupitia kituo cha runinga cha serikali nchini Zimbabwe (ZBC) TV kuwa jeshi lilikuwa limetwaa madaraka na kuwa Rais Robert Mugabe alikuwa salama.

Pia kituo cha radio cha serikali nacho kilitangaza taarifa hiyo ya Jenerali Moyo.

Vituo hivyo havijatangaza matangazo mengine.

Nyingi ya nyimbo hizo ni kuhusu vita vilivyoendeshwa na wapiganaji wa nchi hiyo dhidi ya utawala wa wazungu.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu