Vyama ndugu vya kihafidhina vinavyomuunga mkono kansela wa Ujerumani vyaendelea kuwa na uongozi wa kutosha katika uchunguzi wa maoni ya wapiga kura.

In Kimataifa

Vyama ndugu vya kihafidhina vinavyomuunga mkono kansela wa Ujerumani Angela Merkel vinaendelea kuwa na uongozi wa kutosha katika uchunguzi wa maoni ya wapiga kura uliyochapishwa leo, chini ya miezi sita kabla ya uchaguzi mkuu katika taifa hilo lenye uchumi mkubwa barani Ulaya.
Chama cha siasa za wastani za mrengo wa kushoto cha Social Democrats SPD, kilipata kupanda katika uungwaji mkono katika uchunguzi wa maoni baada ya chama hicho kumchagua spika wa zamani wa bunge la Ulaya Martin Schulz mwezi Januari kuongoza kampeni za chama hicho kumuondoa madarakani Merkel katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Septemba.
Lakini uchunguzi wa maoni ya wapiga kura kutoka mashirika ya INSA na Forsa unaelekeza kwamba kile kilichokuwa kinajulikana kama athari ya Schulz kimepungua wakati chama cha SPD kinaingia katika awamu ngumu ya kampeni kwa ajili ya uchaguzi mwezi ujao, mmoja kati ya chaguzi ndogo katika jimbo la kaskazini la Schleswig-Holtein, na mwingine katika jimbo la North Rhine Westphalia, jimbo lenye watu wengi zaidi nchini Ujerumani.
Uchunguzi huo unaonesha kwamba chama cha kansela Merkel cha CDU na CSU vitapata asilimia 36 wakati SPD itapata asilimia 30

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu