Waandamanaji wavamia Bunge la Macedonia na kushambulia wabunge pamoja na kiongozi wa upinzani.

In Kimataifa

Waandamanaji wamevamia bunge la Macedonia jana, na kuwashambulia wabunge, akiwemo kiongozi wa upinzani, wakipinga kura ya kumchagua spika mpya.
Kiongozi wa chama kikuu cha upinzani cha Social Democrats Zoran Zaev, alionekana akiwa na damu usoni mwake, huku waziri wa mambo ya ndani Agim Nuhiu akisema wabunge 10 walijeruhiwa, pamoja na baadhi ya askari polisi na waandishi habari.
Vurugu hizo zilizuka baada ya waandamanaji karibu 100 wa kizalendo wanaounga chama hasimu cha VMRO-DPMNE, kuingia bungeni wakipeperusha bendera za Macedonia na kuimba wimbo wa taifa.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya ndani, tukio hilo la jana limetokea baada ya chama cha Zaev cha SDSM na wabunge wa asili ya Albania kumchagua spika mpya wa bunge, licha ya spika wa zamani kufunga kikao cha siku.
Spika huyo aliechaguliwa, Talat Xhaferi, ni wa kabila la Albania.
Umoja wa Ulaya ulisema umetiwa matumaini na kuchaguliwa kwa Xhaferi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu