Waandamanaji wavamia Bunge la Macedonia na kushambulia wabunge pamoja na kiongozi wa upinzani.

In Kimataifa

Waandamanaji wamevamia bunge la Macedonia jana, na kuwashambulia wabunge, akiwemo kiongozi wa upinzani, wakipinga kura ya kumchagua spika mpya.
Kiongozi wa chama kikuu cha upinzani cha Social Democrats Zoran Zaev, alionekana akiwa na damu usoni mwake, huku waziri wa mambo ya ndani Agim Nuhiu akisema wabunge 10 walijeruhiwa, pamoja na baadhi ya askari polisi na waandishi habari.
Vurugu hizo zilizuka baada ya waandamanaji karibu 100 wa kizalendo wanaounga chama hasimu cha VMRO-DPMNE, kuingia bungeni wakipeperusha bendera za Macedonia na kuimba wimbo wa taifa.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya ndani, tukio hilo la jana limetokea baada ya chama cha Zaev cha SDSM na wabunge wa asili ya Albania kumchagua spika mpya wa bunge, licha ya spika wa zamani kufunga kikao cha siku.
Spika huyo aliechaguliwa, Talat Xhaferi, ni wa kabila la Albania.
Umoja wa Ulaya ulisema umetiwa matumaini na kuchaguliwa kwa Xhaferi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu