Waasi Nchini Ivory Coast wajeruhi watu sita katika mji wa Bouake.

In Kimataifa
Wanajeshi wanaoasi nchini Ivory Coast wamewajeruhi watu sita katika mji wa pili kwa ukubwa nchini humo wa Bouake wakati huu wasiwasi ukiendelea kushuhudiwa nchini humo kuhusu hatima ya madai yao.
Imethibitishwa kuwa waliojeruhiwa  ni wanaume watano na mama mmoja mwenye watoto watatu.
Watu hao wanaendelea kupata matibabu hospitalini mjini Bouake na imeelezwa kuwa walipata majeruhi hayo baada ya risasi zilizokuwa zinafwatuliwa hewani,  kuingia ndani ya makaazi yao.
Ripoti zinasema kuwa watu wengine 15 walipata majeraha madogo na wanaendelea kupata matibabu.
Wanajeshi hao waliomsaidia rais Allasane Outtara kuingia madarakani mwaka 2010, siku ya Ijumaa walianza kuandamana na kuzingira makao makuu ya jeshi jijini Abidjan wakidai ahadi ya malipo yao kutoka kwa serikali.
Fofana, msemaji wa wanajeshi hao 8,400 alijtokeza na kusema kuwa wanajeshi hao wanaomba radhi na wameachana na mpango wao wa kuendelea kushinikiza kulipwa fedha zao.
Waasi hao wa zamani wanadai kulipwa Euro 18,000 kwa kile mwanajeshi, lakini wamefanikiwa kulipwa Euro 7,500 na ripoti zinasema kuwa ilikuwa imepangwa kuwa watapokea malipo mengine mwezi huu.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu