Waasi wa FARC nchini Colombia wamemaliza rasmi uwepo wa kundi lao.

In Kimataifa

Hatimaye Waasi wa FARC nchini Colombia wamemaliza rasmi uwepo wa kundi hilo kama kundi lililojihami kufuatia mzozo uliodumu nusu karne ambapo zaidi ya watu robo milioni waliuawa.

Akihutubia hafla karibu na mjini Mesetas, kiongozi wa FARC Rodrigo Londono, amesema kuwa shughuli ya kutwaa silaha kutoka kwa kundi hilo imekamilika hatua ambayo itabadilisha sura ya kundi hilo kuwa vugu vugu la kisiasa.

Rais wa Colombia Juan Manuel Santos amesema taifa hilo linasherehekea siku ambayo silaha zilibadilishwa na maneno ya amani.

Mamia ya vipepeo waliachiliwa katika hafla hiyo ambayo pia ilihudhuriwa na maafisa wa serikali na waasi waliyovalia mavazi meupe kama ishara ya amani.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Maagizo ya wizara kuhusu mfuko wa maendeleo ya kilimo.

Naibu Waziri Wa Kilimo Anthony Mavunde, amesema serikaliimeanza kutekeleza uanzishwaji wa mfuko wa maendeleo yakilimo utakaosaidia kukabiliana na changamoto

Read More...

TANZIA: WAZIRI MSTAAFU WA KILIMO AFARIKI DUNIA

Aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini na Waziri wa Kilimo na Mifugo Mhe. Herman Kirigini Amefariki Dunia. Akithibitisha

Read More...

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Professor Makame Mbarawaameliomba Bunge kumuidhinishia kiasi cha Sh Trilioni 3.6ikiwa ni makadirio ya mapato

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu