Waasi wa FARC nchini Colombia wamemaliza rasmi uwepo wa kundi lao.

In Kimataifa

Hatimaye Waasi wa FARC nchini Colombia wamemaliza rasmi uwepo wa kundi hilo kama kundi lililojihami kufuatia mzozo uliodumu nusu karne ambapo zaidi ya watu robo milioni waliuawa.

Akihutubia hafla karibu na mjini Mesetas, kiongozi wa FARC Rodrigo Londono, amesema kuwa shughuli ya kutwaa silaha kutoka kwa kundi hilo imekamilika hatua ambayo itabadilisha sura ya kundi hilo kuwa vugu vugu la kisiasa.

Rais wa Colombia Juan Manuel Santos amesema taifa hilo linasherehekea siku ambayo silaha zilibadilishwa na maneno ya amani.

Mamia ya vipepeo waliachiliwa katika hafla hiyo ambayo pia ilihudhuriwa na maafisa wa serikali na waasi waliyovalia mavazi meupe kama ishara ya amani.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

NACTIVET YASIMAMISHA MAFUNZO CHUO CHA MBEYA TRAINING..DC MALISA AAGIZA KUFANYIWA UHAKIKI VYUO VYOTE WILAYA YA MBEYA

Wazazi Wanafunzi na wahitimu wa chuo cha Mbeya training wameiomba serikali iwasaidie kurudishiwa stahiki zao mara baada ya kubainika

Read More...

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMANNE NOVEMBA 7, 2023

Manchester United na Newcastle United zote zinamfuatilia mshambuliaji wa Lyon Mfaransa Rayan Cherki, 20, ambaye mkataba wake unamalizika Juni

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu