Wabunge wa UKAWA wasusia Bunge.

Wabunge wa Upinzania Bungeni wanaounda Umoja wa Katiba ya Wananchi UKAWA waligoma kuingia ndani ya ukumbi wa Bunge wakati Wabunge 8 wapya wa Viti Maalumu wa CUF wakiapishwa kuchukua nafasi ya Wabunge waliofutwa CUF.

Wabunge hao wamegoma kuapishwa kwa Wabunge hao wapya wakisema kuwa hawakubaliani na hatua hiyo, kwa kuwa haijafuata misingi ya kisheria na wanawaunga mkono wenzao waliofukuzwa.

Antena imenasa sauti ya Mbunge wa Momba Mh David Ernest Linde na hapa anaelezea kuhusiana na wao kugoma kuingia ndani ya Bunge wakati wenzao wanaapishwa.

Tayari wabunge hao wamehapishwa lakini Mh David Ernest ambaye ni katibu wa kambi rasmi Bungeni amesema kuwa, hawatowapa ushirikiano wabunge hao mpaka kesi ya msingi itapokwisha mahakamani.

Na kwa upande wa katibu wa bunge wa CUF MhJuma Hamad, yeye amesema hawakufurahishwa na mchakatako mzima wa kufukuzwa kwa wabunge, ndani ya chama chenye mgogoro  haikufata misingi ya katiba na sheria.

Wabunge ambao wamekula kiapo cha uaminifu leo ni pamoja na  Alfredina Kaigi, Kiza Mayeye, Nuru Bafadhili, Rukia Kassim, Shamsia Mtamba, Sonia Magogo na Zainab Amir.

 

Baada ya kula kiapo hicho cha uaminifu, Spika wa Bunge Job Ndugai akawa na neno kwa wabunge hao na wabunge wengine katika bunge hilo.

 

Exit mobile version