Waendesha Michezo ya kubahatisha watakiwa kulipa kodi TRA.

In Kitaifa

Serikali imewataka waendesha michezo ya kubahatisha na wadau waliokua wakilipa kodi kwenye Bodi ya Michezo Tanzania (Gaming board of Tanzania) kulipa kodi na mawasilisho ya makusanyo yao kwa Kamishna wa Kodi za Ndani wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Hayo yamesemwa mapema hii leo jijini Dar es salaam na Kamishna wa kodi za ndani, Elijah Mwandumbya alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, mbapo amesema kuwa kufuatia mabadiliko ya Sheria ya Fedha namba 4 ya mwaka 2017 yaliyofanywa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye Sheria ya Michezo ya kubahatisha sura namba 166, TRA imepewa jukumu la kukadiria,kukusanya kodi kwenye michezo hiyo kuanzia Julai 1, mwaka huu.

Aidha, Mwandumbya amewataka walipaji kodi hao kuzingatia mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja  na kusajili biashara hizo ili kupatiwa namba ya mlipakodi (TIN) kwa wasiosajiliwa

Naye Mkurugenzi wa Idara ya Elimu kwa Mlipa Kodi, Richard Kayombo amesema kuwa kodi hiyo kwa waendeshaji michezo ya kubahatisha sio kitu kipya ila kilichobadilika ni mahali pa kulipia.

 

 

 

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

ZOEZI LA UOKOAJI HANANG, MAWAZIRI WAFIKA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista J. Mhagama, Waziri wa Ujenzi Innocent

Read More...

RC MBEYA AFANYA UZINDUZI ZOEZI LA UGAWAJI VITAMBULISHO VYA (NIDA)

Mkuu wa mkoa wa mbeya Mhe. Comrede Juma Zuberi Homera amefanya uzinduzi wa wa zoezi la ugawaji wa vitambulisho

Read More...

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu