Wafungwa 17 wapigwa risasi kuuawa nchini Papua new Guinea baada ya kuvunja gereza na kutoroka.

In Kimataifa
  Maafisa wa magereza nchini Papua New Guinea, wamewapiga risasi na kuwauwa wafungwa 17, ambao walivunja gereza na kutoroka siku ya Ijumaa.
Polisi wamewatia mbaroni wafungwa watatu, huku wakiendelea kuwasaka wengine 50 ambao bado hawajulikani waliko tangu kutokea kwa kisa hicho katika gereza la Buimo katika mji wa Lae.
Polisi wanasema kuwa, wengi wa wafungwa waliotoroka walikuwa wahalifu sugu.
Idara ya usalama nchini humo imewatahadharisha raia kuwa macho na watoe taarifa kwa vyombo vya usalama pindi wakiwaona wafungwa hao.
Gereza hilo la Buimo huwa na msongamano mkubwa wa wafungwa na uchafu na mwaka jana wafungwa 12 waliuawa baada ya kujaribu kutoroka.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu