wagombea wawili wa upinzani kupambana na rais Paul Kagame wakati wa Uchaguzi Mkuu mwezi ujao.

In Kimataifa
Tume ya Uchaguzi nchini Rwanda, imewaidhinisha wagombea wawili wa upinzani kupambana na rais Paul Kagame wakati wa Uchaguzi Mkuu mwezi ujao.
Mkuu wa Tume ya Uchaguzi Profesa Kalisa Mbanda amesema wanasiasa hao wawili wa upinzani waliokidhi vigezo vya kuwania urais ni pamoja na Frank Habineza, kutoka chama cha Democratic Green Party na mgombea binafsi Philippe Mpayimana.
Gilbert Mwenedata, Fred Barafinda Skikubo na mwanamke wa pekee Diane Rwigara, hawakufanikwia kuidhinishwa baada ya kukosa kupata saini za wapiga kura 600 kama inavyotakiwa kikatiba.
Tume hiyo mwezi uliopita, iliwapa siku tano wagombea hao kuhakikisha kuwa wanatimiza vigezo hivyo la sivyo wafungiwe kushiriki katika Uchaguzi huo.
Kigezo ambacho hawakutimiza ni kutopata sahihi za wapiga kura 600 kutoka kwa wilaya 12 kati ya 30 nchini humo.
Wagombea binafsi wamekuwa wakilalamikia kusumbuliwa na maafisa wa usalama katika harakati zao za kujitambulisha kwa raia wa nchi hiyo na kueleza mipango yao.
Kampeni zinatarajiwa kuanza katikati ya mwezi huu.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu