Wahadhiri wa vyuo vikuu vya serikali nchini Kenya wasitisha mgomo.

In Kimataifa

Wahadhiri wa vyuo vikuu vya serikali nchini Kenya wamesitisha mgomo baada ya serikali kuahidi kuwalipa zaidi mara moja, kulingana na taarifa za jana za viongozi wa muungano wa wahadhiri wa vyuo vikuu nchini humo.

Wanachama wa Muungano wa Vyuo Vikuu UASU walimaliza mgomo wa siku 54 unaohusu malipo mwezi Febuari na kusaini mkataba na serikali mwezi Machi wa ongezeko la malipo la asilimia 17.5 na asilimi 3.9 katika posho za makaazi.

Lakini walianzisha mgomo mpya mwezi huu juu ya utekelezaji wa malipo hayo waliyokubaliana na serikali.

Muungano wa UASU umesema serikali imetoa kiasi cha shilingi bilioni 5 mwezi huu za kuwalipa wanachama wa muungano huo na hiyo ndiyo sababu ya kusitisha mgomo wao.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu