Wakimbizi zaidi ya 11,000 watumiwa misaada ya kibinadamu na shirika la wakimbizi huko kaskazini mwa Angola

In Kimataifa

Shirika la Wakimbizi la Umoja wa Mataifa, UNHCR, limeanza kutuma msaada wa kibinaadamu kwa wakimbizi zaidi ya 11,000 kaskazini mwa Angola, ambao wanakimbia ghasia Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC.

Umoja wa Mataifa unasema zaidi ya watu milioni moja wamegeuka wakimbizi nchini Congo tangu mapigano yazuke kwenye jimbo la Kasai katikati mwa mwaka jana, huku wengine 25,000 wakivuka kuomba hifadhi nchini Angola.

Msemaji wa UNHCR kusini mwa Afrika, Sharon Cooper, ameliambia shirika la habari la Reuters kwamba ndege ya mizigo ilisafirisha hapo jana shehena ya vyandarua na mablanketi kutokea Dubai.

Uasi wa Kaimuna Nsapu uliozuka katika jimbo la Kasai ya Kati mwezi Agosti mwaka jana umekuwa kitisho kikubwa kwa utawala wa miaka 16 wa Rais Joseph Kabila.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu