Wakimbizi zaidi ya 11,000 watumiwa misaada ya kibinadamu na shirika la wakimbizi huko kaskazini mwa Angola

In Kimataifa

Shirika la Wakimbizi la Umoja wa Mataifa, UNHCR, limeanza kutuma msaada wa kibinaadamu kwa wakimbizi zaidi ya 11,000 kaskazini mwa Angola, ambao wanakimbia ghasia Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC.

Umoja wa Mataifa unasema zaidi ya watu milioni moja wamegeuka wakimbizi nchini Congo tangu mapigano yazuke kwenye jimbo la Kasai katikati mwa mwaka jana, huku wengine 25,000 wakivuka kuomba hifadhi nchini Angola.

Msemaji wa UNHCR kusini mwa Afrika, Sharon Cooper, ameliambia shirika la habari la Reuters kwamba ndege ya mizigo ilisafirisha hapo jana shehena ya vyandarua na mablanketi kutokea Dubai.

Uasi wa Kaimuna Nsapu uliozuka katika jimbo la Kasai ya Kati mwezi Agosti mwaka jana umekuwa kitisho kikubwa kwa utawala wa miaka 16 wa Rais Joseph Kabila.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu