Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Madola kukutana Rwanda

In Kimataifa

Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Madola hatimaye unafanyika jijini Kigali, Rwanda baada ya kuahirishwa mara mbili (2020 na 2021) kwa sababu ya ugonjwa wa Corona.


Mkutano huo unaofanyika kuanzia tarehe 20 hadi 25 Juni 2022 umegawanywa katika makundi mbalimbali kama vile ya vijana, wanawake, wafanyabiashara, Mawaziri wa Mambo ya Nje, Wakuu wa Nchi pamoja na matukio ya pembezoni ambayo kwa pamoja mijadala yake inajikita katika maeneo matano.
Maeneo hayo ni utawala bora, utawala wa sheria, haki za binadamu; vijana, afya, teknolojia na uvumbuzi; maendeleo endelevu na mapambano dhidi ya mabadiliko ya tabianchi.


Mkutano huo unaofanyika kwa kaulimbiu “Kufikia Mustakabali wa Pamoja: Kuunganisha, Kufanya uvumbuzi, Kufanya mabadiliko” (Delivering a Common Future: Connecting, Innovating, Transforming) umejipanga kujadili na kutafutia ufumbuzi wa changamoto zinazozikabili nchi wanachama wa Jumuiya ya Madola ili kufikia maendeleo ya kweli katika nyanja zote.
Tanzania inashiriki kikamilifu katika mkutano huo na kimsingi masuala yanayojadiliwa yanakwenda sanjari na vipaumbele vya Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan.


Ikumbukwe, Rais Samia tangu aingie madarakani, Serikali yake imejipambanua katika kuheshimu haki za binadamu na kuzingatia masuala ya utawala wa sheria na demokrasia. Serikali ya awamu ya sita pia inafanya jitihada mbalimbali zenye lengo la kuyawezesha makundi maalum ya wanawake, vijana na wazee kiuchumi pamoja na kuhakikisha kuwa huduma za afya zinaboreshwa na zinapatikana kwa wananchi wote.


Aidha, mageuzi makubwa ya kiuchumi yameshuhudiwa katika Serikali ya awamu ya sita na uwekezaji mkubwa katika elimu na elimu ya ufundi unaendelea kufanyika` kwa lengo la kuchochea ubunifu bila kusahau mikakati madhubuti ya kukabiliana na madiliko ya tabianchi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu