Wakuu wa wilaya na wakurugenzi watendaji wapewa onyo kuacha kushindana wenyewe kwa wenyewe.

In Kitaifa
WAKUU wa Wilaya  na Wakurugenzi Watendaji  wameonywa kuacha kushindana  wenyewe kwa wenyewe,  na kuendeleza migongano badala isiyo na tija  badala yake  washirikiane kwa kuwa  wanategemeana , katika kutekeleza  Majukumu yao.
Onyo hilo lilitolewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Tamisemi), George Simbachawene mjini Dodoma jana wakati akifungua semina elekezi kwa viongozi hao wa mikoa sita kutoka Kanda ya Ziwa.
Simbachawene  amewataka wachukuliane hali, hisia, tabia na wavumiliane na kushirikiana ,badala ya kuonesheana ubabe na kila mmoja kujiona ana madaraka kuliko mwenzie.
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais (Tamisemi), Mussa Iyombe amewataka  viongozi  hao kujifunza kwa bidii katika semina hiyo, kujua vizuri  Majukumu yao na Mipaka ya kazi yao badala ya kukaa siku tano na kurudi watupu.
Mafunzo hayo  yamewashirikisha  viongozi kutoka mikoa ya Mara, Mwanza, Kagera, Simiyu, Manyara na Geita,

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

NACTIVET YASIMAMISHA MAFUNZO CHUO CHA MBEYA TRAINING..DC MALISA AAGIZA KUFANYIWA UHAKIKI VYUO VYOTE WILAYA YA MBEYA

Wazazi Wanafunzi na wahitimu wa chuo cha Mbeya training wameiomba serikali iwasaidie kurudishiwa stahiki zao mara baada ya kubainika

Read More...

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMANNE NOVEMBA 7, 2023

Manchester United na Newcastle United zote zinamfuatilia mshambuliaji wa Lyon Mfaransa Rayan Cherki, 20, ambaye mkataba wake unamalizika Juni

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu