Wamiliki wa klabu ya Leicester City washtakiwa.

In Kimataifa, Michezo

Wamiliki wa klabu ya Leicester City nchini Uingereza wamedaiwa kushtakiwa kwa umiliki wa £323m zinazodaiwa na serikali ya Thai.

Mahakama ya jinai nchini Bangkok ilikubali kesi dhidi King Power International siku ya Jumatatu , kulingana na shirika la habari la Reuters.

Kesi hiyo pia itawasilishwa dhidi ya maafisa wanaomiliki uwanja wa ndege wa taifa wa Thailand(AOT) Reuters imesema.

BBC imewasiliana na klabu hiyo ya Leicester City FC , King Power na AOT kwa maoni yao.

Makahakama hiyo inailaumu King Power kwa kukosa kuilipa serikali ya Thai bilioni 14 baht (£323m) kutoka kwa operesheni ya kufanya biashara bila kulipa ushuru tangu mwaka 2006.

Kwa kusikilizwa kwa kesi hiyo siku ya Jumatatu , mahakama hiyo ya jinai huko Bangkok iliikubali kesi hiyo na kusema iko tayari kusikiliza upande wa ushahidi mwezi Februari mwaka ujao.

Hatua hiyo dhidi ya kampuni ya King Power, inayomilikiwa na Vichai Srivaddhanaprabha na familia yake iliwasilishwa mwezi Julai.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Serikali kuunga mkono juhudi za Taasisi mbali mbali.

Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Mwinyi, amesema serikaliitaendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Taasisi yaZanzibar Maisha Bora Foundation,pamoja na

Read More...

DKT. KIRUSWA AZINDUA MFUMO WA USHIRIKISHWAJI WA WATANZANIA KATIKA SEKTA YA MADINI

Watanzania waendelea kunufaika Sekta ya Madini, ajira 15,341 zamwagwa, manunuzi ya ndani ya nchi yafikia Dola za Marekani bilioni

Read More...

MAFURIKO YAUWA 190 MALAWI

Takriban watu 190 sasa wamethibitishwa kufariki nchini Malawi baada ya Dhoruba ya Mafuriko ya Tropiki Freddy kulikumba eneo

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu