Wamiliki wa klabu ya Leicester City washtakiwa.

In Kimataifa, Michezo

Wamiliki wa klabu ya Leicester City nchini Uingereza wamedaiwa kushtakiwa kwa umiliki wa £323m zinazodaiwa na serikali ya Thai.

Mahakama ya jinai nchini Bangkok ilikubali kesi dhidi King Power International siku ya Jumatatu , kulingana na shirika la habari la Reuters.

Kesi hiyo pia itawasilishwa dhidi ya maafisa wanaomiliki uwanja wa ndege wa taifa wa Thailand(AOT) Reuters imesema.

BBC imewasiliana na klabu hiyo ya Leicester City FC , King Power na AOT kwa maoni yao.

Makahakama hiyo inailaumu King Power kwa kukosa kuilipa serikali ya Thai bilioni 14 baht (£323m) kutoka kwa operesheni ya kufanya biashara bila kulipa ushuru tangu mwaka 2006.

Kwa kusikilizwa kwa kesi hiyo siku ya Jumatatu , mahakama hiyo ya jinai huko Bangkok iliikubali kesi hiyo na kusema iko tayari kusikiliza upande wa ushahidi mwezi Februari mwaka ujao.

Hatua hiyo dhidi ya kampuni ya King Power, inayomilikiwa na Vichai Srivaddhanaprabha na familia yake iliwasilishwa mwezi Julai.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu